Home »
» Mwigulu nchemba na Nape wachafua hali ya hewa Igunga
Mwigulu nchemba na Nape wachafua hali ya hewa Igunga
Written By Unknown on Sunday, 9 September 2012 | 13:50
Leo Mwigulu na Nape waliitisha mkutano Igunga ambao Mwigulu pekee ndio alifika na kutoa hutuba kwa wananchi, ameongea mengi ambayo hayakuwa na tija kwa wanachi wa Igunga na Taifa labda yalikuwa na tija kwa Chama chake.
Amesema mengi lakini naorodhesha machache aliyozungumza Mh. Mwigulu:
1. Dr. Slaa ni mzinzi na alimpa mimba mtoto wa shule (baada ya kauli hii watu wengi waliondoka kwenye mkutano)
2. Wakialikwa sehemu watu wenye ndoa Dr. Slaa hatahudhuria
3. Kale kazee (Dr. slaa) kanakula kwa kutembea tembea
4. Yule mzee (Dr. slaa) wazee wenzake wamebaki majumbani wanalea wajukuu yeye kuzurura tu
5. CDM wanategemea mtaji wa mauaji katika mikutano yao ?????????
6. Hata kama uchaguzi ukirudiwa igunga lazima washinde kwani timu ni ile ile ya ushindi
7. Lengo la CDM kukata Rufaa ilikuwa ili Kafumu hasiweze kutekeleza Ilani ya CCM
8. Aliuliza wananchi eti kunakosa hata moja Kafumu kalifanya hadi kuvuliwa ubunge ( Walikaa kimya)
9. Kafumu hakufanya kosa lolote - eti kosa nyie kupewa chakula, eti kosa nyie kujengewa daraja
10. Mnamshangilia Dr. slaa wakati ameikimbia Familia
11. Mnamshangilia Kasulumbai mnajua historia yake anakotoka, Akimwangalia tu mtoto wako anakufa.
Jamani hayo ndiyo maneno ya Mwigulu, naomba tuchangie yanatija na mstakabari wa taifa hili?
Nawasilisha
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !